MKAZI WA MOMBA ABEBESHWA KINYESI NA KUZUNGUSHWA MITAANI BAADA KUMKATA SEHEMU ZA SIRI MKEWE
Mkazi wa kata ya Ivuna Kijiji cha kalungu Wilayani Momba anaejulikana kwa jina la Leo Simchimba amebebeshwa kikapu cha kinyesi cha ng'ombe na nguruwe kilichochanganywa na Maji na kupitishwa mitaani na kina mama huku akichapwa viboko baada ya kudaiwa kumjeruhi mkewe sehemu za siri kwa kumkata. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa imekuwa ni desturi kwa Wakazi wa Momba pindi unapokutwa na makosa kushitakiwa kwa Viongozi wa Kimila hivyo wao ndio hutoa adhabu zikiwemo faini ama kuzungushwa mitaani kwa kubebeshwa kinyesi kilicholewesha na kupigwa viboko. "Huyu bwana alimdhalilisha kwa kumkata kiungo cha Mkewe sehemu za siri kwa Wivu wa mapenzi na kisha kumpiga pia Wananchi waliokwenda kuamlia ugomvi aliwatishia na kuanza kuwatukana Wana mtaa hivyo tukaamua kwenda kumshitaki kwa Wazee wa Kimila na ndipo walipotoa adhabu ya kubebeshwa kinyesi na kuzungushwa Kijiji kizima na adhabu zingine kama kulipa Mbuzi,Unga na pombe pamoja na fedha"alisema mmoja wa mas...