DARAJA MUHIMU WILAYANI MOMBA LABOMOKA
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amesema Serikali inafunga daraja la Chuma la Kijeshi kwenye daraja la Yara ambalo lilivunjika katika msimu wa mvua 2020/2021 na kupelekea magari makubwa kushindwa kupita.
Mkuu wa Mkoa amesema daraja litafungwa muda wowote baada ya taratibu za Kijeshi kukamilika.Daraja la Yara linaunganisha mawasiliano Kati ya Chitete na Kamsamba ambapo Mabasi ya abiria na Maloli ya Mizigo hutumia daraja hilo.
MWISHO.
Maoni