WANANCHI SONGWE WAZINGIRA KITUO CHA POLISI KUDAI MIKOBA WA RAMBARAMBA WAO
Kundi la wananchi wa kijiji cha Chang'ombe katika wilaya ya Songwe, wamevamia kituo cha Polisi Galula wakishinikiza kurejeshewa mikoba ya waganga wa jadi (lambalamba) iliyokamatwa na askari wa kituo hicho.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Janneth Magomi amesema wananchi hao walizingira kituo hiho Leo alfajiri kufuatia askari kuvamia kijiji hicho ili kuzuia waganga hao kufanya operasheni ya kukamata wachawi.
Amesema kufuatia tukio hilo Mwenyekiti wa kijiji na watu wengine 23 wanashikiriwa na jeshi hilo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Maoni