Tarehe ya Kuzaliwa: 05 Novemba, 1973 Mahali: Kijiji cha Isale, Wilaya ya Mbulu, Mkoa wa Manyara ELIMU Mh. Ester Alexander Mahawe alianza safari yake ya elimu katika Shule ya Msingi Upper Kitete, Wilaya ya Karatu mnamo 1982-1983 na baadaye kuhamia Shule ya Msingi Isale, ambako alihitimu mwaka 1988. Alipata elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Imboru, Wilaya ya Mbulu kati ya mwaka 1989-1992. Mnamo 1994-1996, alihitimu mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti kutoka Chuo cha Ualimu Monduli, Mkoa wa Arusha. Mwaka 2012-2013, alihitimu stashahada ya Uongozi na Utawala kutoka Chuo cha ESAMI, Mkoa wa Arusha. NDOA NA FAMILIA Mnamo tarehe 17 Septemba 2005, Ester Alexander Mahawe alifunga ndoa na Alexander Samson. Ndoa yao ilijaliwa watoto watatu wa kuwazaa: wavulana wawili na msichana mmoja. Aidha, aliwalea watoto wengine sita na hivyo kuacha jumla ya watoto tisa pamoja na wajukuu tisa. KAZI NA UZOEFU Huduma ya Ualimu: 1996-1997: Mh. Ester alikuwa mwalimu katika St. Constantine International Sch...
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Afya, Dk Festo Dugange amesema takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano bado ni kikubwa ambapo kwa Mkoa wa Kigoma ni asilimia 27.1, Katavi asilimia 32.2, Njombe asilimia 50.4, Songwe asilimia 31.9 na Rukwa asilimia 49.8. Amesema hayo katika hafla ya kusaini hati za makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa lishe unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID) iliyofanika leo Mei 07, 2024 katika Ukumbi wa Sokoine jijini Dodoma. Dk Dugange amesema viwango vya matatizo ya lishe nchini vimeendelea kupungua mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka 2022 kiwango cha udumavu nchini ni asilimia 30 ikilinganishwa na asilimali 34 mwaka 2015. Aidha, naibu waziri huyo amesema tunapaswa kuendelea kuhamasisha ulaji wa chakula mchanganyiko chenye virutubisho na kuzingatia mtindo bora wa maisha. “tuweke kipaumbele katika kuimarisha usafi wa mazin...
karibu nawe, maana ni moja ya viashiria vya dharau na majivuno. Mtu anayeringa hana rafiki na taratibu atajikuta akigombana na kila mtu na baadaye atajikuta anaishi kwenye dunia ya peke yake. MASENGENYO Kusengenya wengine ni tabia isiyokubalika na jamii. Kwa bahati mbaya sana ni kwamba, msengenyeji huwa hajui kama ana tabia hiyo. Ilivyo ni kwamba, mtu anayesengenya wengine hujisahau. Leo akiwa mahali anamsema fulani, kesho atakwenda kuzungumza na yule aliyemsengenya jana, akimsengenya mwingine. Taarifa za usengenyaji zikisambaa, mwishowe anajikuta akiwa hakubaliki tena na watu wanaomzunguka. Anashangaa ghafla anaishi kwenye dunia ya peke yake. Hakuna anayemkubali. Akitokea mahali, wenzake wanainuka na kumuacha peke yake. Alama hii ikuzindue usingizini na ukae mbali na usengenyaji ili usijitengenezee mazingira ya kutokubalika kwenye jamii unayoishi. KUTOJITOA Kuna watu wana tabia za ajabu sana… yanapotokea mambo kwenye jamii hana muda wa kushiriki. Hili ni tatizo kubwa na husababi...
Comments