Katibu wa siasa na uenezi wilaya ya mbozi Zawadi Shombe amechukua fomu ya kutetea kiti chake cha Uenezi Wilaya ya Mbozi katika Uchaguzi unoatarajia Kufanyika mwanzoni mwa mwezi wa kumi.
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Afya, Dk Festo Dugange amesema takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano bado ni kikubwa ambapo kwa Mkoa wa Kigoma ni asilimia 27.1, Katavi asilimia 32.2, Njombe asilimia 50.4, Songwe asilimia 31.9 na Rukwa asilimia 49.8. Amesema hayo katika hafla ya kusaini hati za makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa lishe unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID) iliyofanika leo Mei 07, 2024 katika Ukumbi wa Sokoine jijini Dodoma. Dk Dugange amesema viwango vya matatizo ya lishe nchini vimeendelea kupungua mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka 2022 kiwango cha udumavu nchini ni asilimia 30 ikilinganishwa na asilimali 34 mwaka 2015. Aidha, naibu waziri huyo amesema tunapaswa kuendelea kuhamasisha ulaji wa chakula mchanganyiko chenye virutubisho na kuzingatia mtindo bora wa maisha. “tuweke kipaumbele katika kuimarisha usafi wa mazin...
Mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara Mkoa wa Songwe TCCIA Charles Chenza ameomba Vituo vya kusimamishia magari vya Senjele na Nanyala vilivyopo Wilayani Mbozi viondolewe kwani vimekuwa ni kero kwa Wafanyabiashara na Wananchi kwa ujumla kutokana na kukaa muda mrefu wakisubiri foleni ya kupishana magari makubwa na madogo Akiongea katika kikao cha baraza la Biashara la Mkoa wa Songwe lililofanyika katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Songwe leo 24 Mei 2024 Chenza amedai kuwa kumekuwepo na usumbufu usiokuwa na ulazima wowote wa watu kukaa muda mrefu katika foleni hiyo hivyo amemuomba Mkuu wa Mkoa Daniel Chongolo kama Mwenyekiti wa Usalama Mkoa wa Songwe kuwasaidia kero hiyo. Akijibu kwa niaba ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe SACP Augustino Senga afisa mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Songwe Kamanda ACP Gallus Hyera amesema wao kama polisi kwa kuwa kituo vituo hivyo vinalalamikiwa watakwenda kujadiliana ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa magari kukaa katika foleni hiyo....
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Daniel Chongolo Amekasilishwa na kitendo cha Kutokuwepo katika ziara yake Tunduma kwa Wakuu wa Idara za RUWASA na TANESCO kusikiliza na kutatua kero za Wananchi. Katika ziara ya kikazi iliyofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Tunduma, hali ya sintofahamu ilijitokeza baada ya wakuu wa idara muhimu za RUWASA na TANESCO kushindwa kufika ambapo Ambapo Chongolo alieleza kutoridhishwa kwake na kitendo cha viongozi hao kutohudhuria ziara hiyo na kumuagiza Katibu Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Happiness Seneda kuhakikisha Wakuu hao ziara zake wanakuwepo na kama hawawezi kusikiliza kero za Wananchi basi watafute Mkoa mwingine wa kufanya kazi. Katika hotuba yake mbele ya maafisa na wananchi waliokuwepo, mkuu wa mkoa alisisitiza umuhimu wa viongozi wa taasisi za umma kuwajibika na kuheshimu ratiba za ziara za kikazi, hasa pale zinapohusisha masuala ya huduma za msingi kama maji na umeme, ambazo ni muhimu kwa maendeleo ya wananchi. Alieleza kwamba kitendo cha kutokuwep...
Maoni