NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Afya, Dk Festo Dugange amesema takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano bado ni kikubwa ambapo kwa Mkoa wa Kigoma ni asilimia 27.1, Katavi asilimia 32.2, Njombe asilimia 50.4, Songwe asilimia 31.9 na Rukwa asilimia 49.8. Amesema hayo katika hafla ya kusaini hati za makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa lishe unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID) iliyofanika leo Mei 07, 2024 katika Ukumbi wa Sokoine jijini Dodoma. Dk Dugange amesema viwango vya matatizo ya lishe nchini vimeendelea kupungua mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka 2022 kiwango cha udumavu nchini ni asilimia 30 ikilinganishwa na asilimali 34 mwaka 2015. Aidha, naibu waziri huyo amesema tunapaswa kuendelea kuhamasisha ulaji wa chakula mchanganyiko chenye virutubisho na kuzingatia mtindo bora wa maisha. “tuweke kipaumbele katika kuimarisha usafi wa mazin...
MBUNGE wa Jimbo la Momba Mkoani Songwe Mhe. Condester Sichalwe (Mundy) ametenga kiasi cha shilingi milioni 28 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa ofisi za CCM kwenye kata zote 14 za jimbo hilo. Akizungumza kwa nyakati tofauti kwenye vikao vya Halmashauri Kuu ya CCM kata za Nkangamo na Msangano, Mbunge Sichalwe amesema lengo la kutoa fedha hizo ni kuunga mkono shughuli za maendeleo za kujenga chama hicho. Akiwa mgeni mualikwa kwenye kikao hicho katibu wa CCM wilaya ya Momba Kataba Sukuru, amempongeza na kumshuru Mbunge Condester Schalwe kwa kutoa fedha hizo kwa madai kuwa anajenga chama kwa vitendo. “Tukushuru sana Mheshimiwa Mbunge jambo hili unalofanya nikubwa sana, kutoa milioni mbili kila kata si jambo dogo, inaonyesha ni jinsi gani unavyokipenda chama chetu, hakika wewe ni Mbunge wa mfano sana” Kataba. Kupitia mpango huo tayari Mbunge ametoa milioni Nne kwa kata mbili za Nkangano na Msangano, huku akiendelea na kata zingine, lengo ni kuona kata zote zinafikiwa na fedha hizo.
Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi limewapongeza wanafunzi wa darasa la saba kwa kufanya vizuri na kuazimia kianzisha programu za mitihani ya wiki ikiwa ni mkakati wa kupandisha kupandisha ufaulu. Akizungumza katika kikao hicho cha Baraza la kupokea taarifa za Kata Mwanyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mhe. George Musyani amesema kuwa jitihada zilizofanywa na wataalamu kupandisha ufaulu zinatakiwa kutiliwa mkazo ili kuongeza kiwango cha ufaulu. "Tutengeneze mkakati ambao tutakwenda nao mpaka mwakani ili watoto wetu wafaulu zaidi. Nawashukuru walimu kwa jitihada zao zilizowafanya wanafunzi hao kuongeza ufaulu kutoka asilimia 74 mpaka asilimia 81" amesema na kuongeza; "Twendeni kianzisha programu za mitihani ya kila mwisho wa wiki ambayo inaweza kufanyika kwa kushindanisha shule kwa shule ambayo itawafanya wasome kwa bidii. Tujitahidi kwenda kutoa elimu kwa wananchi wetu kuhusiana na suala hili ili wote tuwe na uelewa wa pamoja ili kusitokee manung...
Maoni