DC MAHAWE AONYA WANAOHARIBU VYANZO VYA MAJI
Mkuu huyo wa Wilaya ametoa maagizo hayo leo Jumatatu Juni 5, 2023 wakati akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kiwilaya yamefanyika Kijiji cha Nambala kata ya Mlowo wilayani humo.
Amesema kuwa maji yanapokuwa changamoto wanawake na watoto ndio wanaathirika kwa kiasi kikubwa hasa kwa kutafuta nishati hiyo.
"Msisahau kuwa maji yanapokuwa changamoto wanamama na watoto ndio wanapata shida kwenda kutafuta maji"
Amesema lengo la Rais Samia Suluhu Hassan ni kumtua ndoo mama kichwani kwa kuwasogezea huduma ya maji karibu ili muda wanaotumia kutafuta maji wautumie kwenye shughuli za uzalishaji.
"Maelekezo niliyotoa yazingatiwe, tutunze vyanzo vya maji".
DC huyo amesema kuwa wilaya hiyo ina bahati ya kuwa na vyanzo vingi vya maji lakini changamoto moja ni kubwa iliyopo ni kutokutunza vyanzo hivyo.
"Hali ya maji kwa wilaya ya Mbozi ikiwa hatutalinda vyanzo hivi miaka isiyozidi 10 tukienda hali hii tutakosa maji" amesisitiza
Amewataka wanaolima kwenye vyanzo vya maji kuacha tabia hiyo kwa kuwa ndio chanzo cha kukausha vyanzo hivyo.
"Hali ya upatikanaji wa maji sio nzuri. Mnaweza msiione leo lakini siku zinakuja mtaomboleza. Maji hayana mbadala. Tutunze hivi vyanzo" ametahadharisha mkuu huyo wa wilaya.
"Babu zetu wasingevitunza hivi vyanzo sisi tusingevikuta, kila mtu akilima kwenye vyanzo vya maji pakikauka tutakwenda kulima wapi" amehoji DC huyo.
Katika maadhimisho hayo yaliyoongozwa na mkuu wa wilaya, miti 1000 imepandwa katika chanzo cha maji cha Nambala.

Maoni