RAIS SAMIA ATENGUA UTEUZI WA KATIBU WA WIZARA YA MAJI
Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu Wizara ya Maji Nadhifa Kemikimba.
Kemikimba aliteuliwa kushika nafasi hiyo Februari 26, 2023 na aliapishwa kushika wadhifa huo katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma Februari 27, 2023.
Awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo na amewahi pia kutumikia nafasi mbalimbali ikiwamo Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Ubora wa Maji.
Taarifa ya kutenguliwa kwake imetolewa leo Ijumaa Agosti 18, 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zuhura Yunus

Maoni