DED MOMBA APONGEZWA NA BARAZA LA MADIWANI KWA UKUSANYAJI MAPATO

Baraza la Madiwani limekutana Kujadili hesabu za mwisho kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Na limepitisha hesabu hizo.

Mkutano huo umefanyika leo tar Septemba 29. 2024 katika ukumbi wa mkutano wa Halmashauri. 

Katika mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba Mhe. Mathew Chikoti amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri pamoja na watumishi wote kwa juhudi na umoja waliouonesha katika ukusanyaji wa mapato.


Juhudi hizo zimefanya kuwa na Makusanyo kwa 168% ikiwa 

Makisio yalikuwa Bilion 1.8 na kiasi kilichokusanywa ni Bilioni 3.1 sawa na zidio la Bilioni 1.3.

'Madiwani na watumishi wote kwa pamoja tusimamie ukusanyaji wa mapato' amesema Chikoti.

Comments

Popular posts from this blog

UDUMAVU BADO TISHIO -DUGANGE

CONSTRUCTION OF THE ISONGOLE-ISOKO ASPHALT ROAD IS NOW OFFICIAL, CONTRACTOR INTRODUCED TO THE PUBLIC

MBUNGE MOMBA KUTOA SHILINGI MILIONI 28 UJENZI WA OFISI ZA CCM KATA 14