Posts

Showing posts from January, 2025

KUMBUKUMBU YA MAISHA YA MH. ESTER ALEXANDER MAHAWE

Image
Tarehe ya Kuzaliwa: 05 Novemba, 1973 Mahali: Kijiji cha Isale, Wilaya ya Mbulu, Mkoa wa Manyara ELIMU Mh. Ester Alexander Mahawe alianza safari yake ya elimu katika Shule ya Msingi Upper Kitete, Wilaya ya Karatu mnamo 1982-1983 na baadaye kuhamia Shule ya Msingi Isale, ambako alihitimu mwaka 1988. Alipata elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Imboru, Wilaya ya Mbulu kati ya mwaka 1989-1992. Mnamo 1994-1996, alihitimu mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti kutoka Chuo cha Ualimu Monduli, Mkoa wa Arusha. Mwaka 2012-2013, alihitimu stashahada ya Uongozi na Utawala kutoka Chuo cha ESAMI, Mkoa wa Arusha. NDOA NA FAMILIA Mnamo tarehe 17 Septemba 2005, Ester Alexander Mahawe alifunga ndoa na Alexander Samson. Ndoa yao ilijaliwa watoto watatu wa kuwazaa: wavulana wawili na msichana mmoja. Aidha, aliwalea watoto wengine sita na hivyo kuacha jumla ya watoto tisa pamoja na wajukuu tisa. KAZI NA UZOEFU Huduma ya Ualimu: 1996-1997: Mh. Ester alikuwa mwalimu katika St. Constantine International Sch...

*KUNDO AGOMA KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI VWAWA-MLOWO

Image
  Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, amegoma kuweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa Vwawa-Mlowo uliopo Mkoani Songwe, unaotekelezwa na Mkandarasi Mzawa wa kampuni ya Current Construction Ltd ya Jijini Dar es salaam  mpaka changamoto zilizopo zitakapo tatuliwa. Mhandisi Kundo amesema kuwa, changamoto hizo ni pamoja na  kazii kufanyika chini ya kiwango kilichokubaliwa.  Kufuatia hali hiyo, Mhandisi Kundo ameiagiza bodi ya Vwmwassa na RUWASA kuhakikisha kwamba wanamsimamia mkandarasi huyo,  ili aweze kufanya marekebisho kwa kasoro zote zilizobainika. Mhandisi Kundo amechukua uamuzi huo leo Januari 14, 2025 katika siku ya pili ya ziara yake ya siku mbili Mkoani Songwe, baada ya kusomewa taarifa ya maendeleo ya utekeleza kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vwawa-Mlowo (Vwamwassa), Mhandisi Clavery Casmir. "Niko tayari kupewa majina mabaya, lakini kwa mradi huu siwezi kuweka jiwe la msingi mameneja wa Wilaya, hata ...

NAIBU WAZIRI WA MAJI AZINDUA VISIMA VILIVYOJENGWA NA MBUNGE MWENISONGOLE MILIONI 65

Image
Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, amezindua mradi wa visima viwili vilivyojengwa kwa juhudi za Mbunge wa Jimbo la Mbozi, Mheshimiwa George Mwenisongole, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali. Visima hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 65 vimejengwa katika vijiji vya Ileya na Sambewe vilivyopo Kata ya Itumpi, na vinatarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 4,068. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mbunge Mwenisongole alimshukuru Naibu Waziri kwa kukubali mwaliko wake na kuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi hiyo kutembelea vijiji hivyo tangu uhuru. Alisema visima hivyo ni sehemu ya juhudi za kuunga mkono kampeni ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama ndoo kichwani. "Niliona mateso ya wananchi wangu, hususan kina mama waliokuwa wakitegemea maji ya mvua kwa msimu mzima. Leo hii tumewapa suluhisho la kudumu kwa visima hivi, ambavyo ni historia kwao. Natoa shukrani kwa wadau wote waliosaidia kufanikisha mradi huu," alisema Mwenisongole. Kwa upande wake, ...

TABIA ZINAZOWEZA KUKUFANYA USIKUBALIKE KWA JAMII

Image
  karibu nawe, maana ni moja ya viashiria vya dharau na majivuno. Mtu anayeringa hana rafiki na taratibu atajikuta akigombana na kila mtu na baadaye atajikuta anaishi kwenye dunia ya peke yake. MASENGENYO Kusengenya wengine ni tabia isiyokubalika na jamii. Kwa bahati mbaya sana ni kwamba, msengenyeji huwa hajui kama ana tabia hiyo. Ilivyo ni kwamba, mtu anayesengenya wengine hujisahau. Leo akiwa mahali anamsema fulani, kesho atakwenda kuzungumza na yule aliyemsengenya jana, akimsengenya mwingine. Taarifa za usengenyaji zikisambaa, mwishowe anajikuta akiwa hakubaliki tena na watu wanaomzunguka. Anashangaa ghafla anaishi kwenye dunia ya peke yake. Hakuna anayemkubali. Akitokea mahali, wenzake wanainuka na kumuacha peke yake. Alama hii ikuzindue usingizini na ukae mbali na usengenyaji ili usijitengenezee mazingira ya kutokubalika kwenye jamii unayoishi. KUTOJITOA Kuna watu wana tabia za ajabu sana… yanapotokea mambo kwenye jamii hana muda wa kushiriki. Hili ni tatizo kubwa na husababi...