WAZIRI AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MLINZI WAKE


 Charles Okello Engola ni Waziri wa Kazi, Ajira na Uhusiano wa Viwanda wa Nchini Uganda ambaye anadaiwa kuuawa asubuhi ya hii leo Mei 02, 2023 kwa kupigwa risasi na mlinzi wake.

Kwa mujibu wa Naibu Msemaji wa Polisi, Luke Owoyesigire, tukio hilo limetokea asubuhi ya leo.
Imeelezwa kuwa Waziri Okello alikuwa anatoka nyumbani kwenda kazini na ndipo ghafla mlinzi wake binafsi akampiga risasi kisha akaanza kupiga risasi juu huku akikimbiakimbia mitaani.

Msemaji huyo ameeleza kuwa mlinzi huyo amesikika akisema hajalipwa mshahara kwa muda mrefu.
“Ni kweli. Nendeni Kyanja. Mlinzi amemuua bosi wake,” Luke Owoyesigire.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UDUMAVU BADO TISHIO -DUGANGE

WAFANYABIASHARA SONGWE WALALAMIKA FOLENI YA KUSIMAMISHIA MAGARI SENJELE NA NANYALA WILAYANI MBOZI

CHONGOLO AWACHARUKIA RUWASA NA TANESCO KUTOSHIRIKI ZIARA YAKE