MKUU WA POLISI AHUKUMIWA KUNYONGWA

 MAHAKAMA ya Iran, imemuhukumu kifo Mkuu wa Polisi kaskazini mwa Iran baada ya kushtakiwa kwa kuua mtu wakati wa maandamano yaliyotokea nchini humo mwaka 2022.


Vyombo vya habari vya ndani vimeripoti kuwa, Mkuu wa Polisi, Jafar Javan mardi, alikamatwa mwezi Desemba mwaka 2022 kutokana na mauaji ya mwandamanaji wakati wa maandamano makubwa yaliyochochewa na kifo cha Mahsa Amini akiwa chini ya ulinzi wa polisi.

Amini mwenye umri wa miaka 22, alifariki mwezi Septemba 2022 akiwa chini ya ulinzi wa polisi kufuatia kukamatwa kwake kwa madai ya kukiuka sheria kali ya nchi kuhusu mavazi kwa wanawake.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UDUMAVU BADO TISHIO -DUGANGE

MBUNGE MOMBA KUTOA SHILINGI MILIONI 28 UJENZI WA OFISI ZA CCM KATA 14

BARAZA LA MADIWANI LAWAPONGEZA WALIMU UFAULU WA DARASA LA SABA