Posts

Showing posts from December, 2024

MWILI WA BINTI ALIEBAKWA Rucu WAZIKWA KWAO ILEJE

Image
 Mwili wa Rachael Mkumbwa wazikwa Ileje Baba mzazi wa marehemu aliangukia jeshi la polisi Denis Sinkonde.,Mwananchi Denissinkonde@mwananchi.co.tz Ileje. Wakati mwili wa Rachael Mkumbwa ukizikwa leo katika kjiji cha Isongole kata ya Isongole wilayani Ileje Mkoani Songwe baba mzazi wa binti huyo Dickinson Mkumbwa ameliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina kuwakamata waliohusika kuhusika na mauaji hayo. Dickinson Mkubwa amesema licha ya mwanangu kuzikwa Leo naiomba serikali kupitia jeshi la polisi lifanye uchunguzi kuwabaini na kuwakamata wahusika wote ili Sheria ifuate mkondo wake na kukomesha vitendo vya ubakaji. Amesema unyama aliofanyiwa mwanae ni kitendo ambacho hakivumiliki kwani mwanae alikuwa akiishi kwa kumtumikia Mungu lakini amefariki katika mazingira ambayo hayastahikili mioyo yetu. Mkumbwa amesema kama familia wanategemea jeshi la polisi na serikali katika upelelezi ambao utasaidia kuwakamata waliohusika kutenda unyama huo kwani familia ya Racho imeumizwa na taar...

AJALI YA GARI WILAYANI SONGWE YAUA WATATU, YAJERUHI 15

Image
 AJALI YA GARI SONGWE YAUA WATATU, YAJERUHI 15 Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limetoa taarifa kuhusu ajali mbaya ya barabarani iliyotokea Desemba 13, 2024, majira ya saa 12:30 jioni. Ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Mitsubishi Fuso Basi lenye namba za usajili T.701 DEN, mali ya Kampuni ya Mwalumengese. Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, gari hilo lilipata hitilafu baada ya kupasuka kwa tairi la nyuma, hali iliyosababisha gari hilo kuacha njia, kupinduka, na kupelekea vifo vya watu watatu na majeruhi 15. Mahali na Chanzo cha Ajali Ajali ilitokea katika Barabara ya Mkwajuni-Mbalizi wilayani Songwe. Dereva wa gari, Omary Ally Mdachi (45), ambaye ni mkazi wa Mkwajuni, alifariki dunia papo hapo. Watu Waliopoteza Maisha Jeshi la Polisi limewataja waliopoteza maisha katika ajali hiyo kuwa ni: 1. Omary Ally Mdachi (45) – Dereva wa gari, mkazi wa Mkwajuni. 2. Lugano Mwakasole Asangalwisye (25) – Mkulima, mkazi wa Saza, Wilaya ya Songwe. 3. Mwanamume mmoja ambaye bado hajafahamika, ...

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA "MAMA SAMIA" KUZINDULIWA MKOANI SONGWE KESHO

Image
  Songwe, Desemba 12, 2024 – Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe inatarajia kuzindua rasmi Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya "Mama Samia Legal Aid Campaign" (MSLAC). Uzinduzi huu umefanyika katika viwanja vya CCM Vwawa na unatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika kutoa haki na msaada wa kisheria kwa wakazi wa mkoa huu. Akizungumza kwa Niamba ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mkuu wa Wilaya ya Ileje Farida Mgomi katika Kikao na Waandishi wa habari aliwahimiza wananchi wa Songwe kuchangamkia fursa hii adimu ya kupata msaada wa kisheria bure. "Haki za msingi za binadamu hazipaswi kupuuzwa. Kampeni hii inalenga kutoa msaada wa kisheria kwa waathiriwa wa ukatili wa kijinsia, unyanyasaji, na wale waliokosa fursa ya kutetea haki zao," alibainisha. Kampeni ya "Mama Samia Legal Aid Campaign" inalenga kuongeza ufahamu wa sheria kama chombo muhimu cha kulinda haki za binadamu.Kutoa msaada wa kisheria kwa waathiriwa wa vitendo vya u...

BONANZA LA MICHEZO MOROGORO LAHAMASISHA KUPINGA UKATILI KWA WAFANYAKAZI WA NDANI

Image
Mtaa wa Shule, Kata ya Chamwino, Manispaa ya Morogoro, uligeuka kitovu cha mshikamano na hamasa, wakati Bonanza la Michezo lenye lengo la kuendeleza juhudi za kupinga ukatili wa kijinsia kwa wafanyakazi wa ndani lilipofanyika leo. Tukio hili la kipekee liliandaliwa na Taasisi ya The Light for Domestic Workers na kuhudhuriwa na mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwanamke na Mafanikio, Bi. Maria Mapunda. Katika hotuba yake, Bi. Mapunda aligusia masuala muhimu kuhusu haki na ustawi wa wafanyakazi wa ndani. Alisisitiza umuhimu wa mikataba ya maandishi, malipo sahihi na kwa wakati, pamoja na kuwajengea mazingira ya kazi yenye upendo, heshima, na thamani. Aidha, alieleza kuwa mafunzo ya awali kwa wafanyakazi wa ndani yanapaswa kuwa kipaumbele ili kupunguza makosa ya mara kwa mara kazini. "Ni wajibu wetu kama jamii kuhakikisha tunawalinda na kuwaendeleza wafanyakazi wa ndani. Wanapaswa kulipwa stahili zao kwa haki, kuelekezwa majukumu yao, na kupendwa kama binadamu wengine. Ukatili wa...