MWILI WA BINTI ALIEBAKWA Rucu WAZIKWA KWAO ILEJE

Mwili wa Rachael Mkumbwa wazikwa Ileje Baba mzazi wa marehemu aliangukia jeshi la polisi Denis Sinkonde.,Mwananchi Denissinkonde@mwananchi.co.tz Ileje. Wakati mwili wa Rachael Mkumbwa ukizikwa leo katika kjiji cha Isongole kata ya Isongole wilayani Ileje Mkoani Songwe baba mzazi wa binti huyo Dickinson Mkumbwa ameliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina kuwakamata waliohusika kuhusika na mauaji hayo. Dickinson Mkubwa amesema licha ya mwanangu kuzikwa Leo naiomba serikali kupitia jeshi la polisi lifanye uchunguzi kuwabaini na kuwakamata wahusika wote ili Sheria ifuate mkondo wake na kukomesha vitendo vya ubakaji. Amesema unyama aliofanyiwa mwanae ni kitendo ambacho hakivumiliki kwani mwanae alikuwa akiishi kwa kumtumikia Mungu lakini amefariki katika mazingira ambayo hayastahikili mioyo yetu. Mkumbwa amesema kama familia wanategemea jeshi la polisi na serikali katika upelelezi ambao utasaidia kuwakamata waliohusika kutenda unyama huo kwani familia ya Racho imeumizwa na taar...