AGIZO LA WAZIRI WA UJENZI LATEKELEZWA KWA VITENDO SONGWE

Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) imetekeleza kwa mafanikio maagizo ya Wizara ya Ujenzi yanayolenga kupunguza changamoto ya msongamano katika barabara ya TANZAM, hususan eneo la Tunduma, maagizo ambayo yalitolewa Novemba 18, 2024 na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Innocent Meneja wa TANROADS Mkoa wa Songwe, Mhandisi Suleiman Bishanga, amesema juhudi hizo ni matokeo ya mwongozo uliotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Innocent Bashungwa. "Waziri alitoa maagizo ya kutafuta suluhisho la haraka, na kwa kushirikiana na TANROADS Mkoa wa Mbeya, tumefanikisha kupunguza msongamano mkubwa uliokuwa ukisababisha usumbufu kwa madereva," alisema Mhandisi Bishanga. Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuweka mizani ya ziada inayohamishika (mobile weighbridge) kwa ajili ya kupima magari yanayotoka Tunduma kwenda Dar es Salaam, uimarishaji wa usi...