Machapisho

PICHA MBALI MBALI ZA KUAGANA NA KUWAKARIBISHA DED NA DAS WAPYA ILEJE

Picha
 

TIMU YAUNDWA KUKABILIANA NA FORENI TUNDUMA

Picha
SONGWE: Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis Michael ameunda timu maalumu  ambayo itakuwa na kazi ya kutatua foleni ya Malori iliyopo katika Mji wa Tunduma, timu hiyo ni kutoka kwa madereva ambao watawakilishwa na vyama vyao, TANROADS, TRA, Jeshi la Polisi (RTO) na mawakala. Mkuu wa Mkoa ameunda timu hiyo baada ya kufanyika kikao kazi cha utatauzi wa foleni ya Malori kilichowakutanisha viongozi kutoka vyama vya madereva, wamiliki wa Malori, Mawakala wanaovusha magari, Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), Wakala wa Barabara (TANROADS) Songwe, Jeshi la Polisi pamoja na viongozi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Wilaya ya Momba kilichofanyika ofisini kwake, Juni 14. Mkuu wa Mkoa amesema timu aliyoiunda inatakiwa kuwasilisha mapendekezo, maoni  ya muda mfupi na ya muda mrefu kuhusu utatauzi wa foleni ya Malori kwa kuwa wao ndio wanazijua changamoto vizuri. "Kuna changamoto ambazo ziko ndani ya uwezo wetu hapa, hivyo nendeni mfanye kazi kwa pamoja na mje na majibu sahihi ya nini tu...

AFUFUKA NA KUPIGA JENEZA KWA MIKONO AOKOLEWE

Picha
 Mwanamke wa makamo kutoka Ecuador aliyezinduka baada ya madaktari kutangaza kuwa amefariki, anapatiwa matibabu katika hospitali ya serikali ambayo ilitangaza kuwa amekufa siku mbili zilizopita, mtoto wake alisema Jumapili. Video iliyotumwa kwenye Twitter inamuonyesha Bella Montoya, 76, kwenye jeneza likiwa wazi akipumua kwa nguvu huku wanaume wawili wakimsaidia. Mtoto wake, Gilbert Balberán, alisema "alikuwa akipiga sanduku" kwa mkono wake wa kushoto baada ya kuamka kwa saa tano. Balberán alilazimika kuomba mchango wa jeneza kwa familia maskini baada ya hospitali hiyo, kutangaza kuwa Montoya amekufa siku ya Ijumaa. "Hata walitupa cheti cha kifo," alisema kwenye video iliyotangazwa na vyombo vya habari vya ndani. Vyombo vya habari vya Ecuador viliripoti tukio hilo lisilo la kawaida, na vichwa vya habari vikisheheni ‘kufufuka’ kwa mwanamke huyo. "Mama yangu amepata oksijeni. Moyo wake uko shwari. Daktari alimfinya mkono wake na akaitikia," Balberán alisema ...

AFARIKI WAKISHINDA KUNYWA POMBE, WANNE WALAZWA

Picha
 Mtu mmoja amefariki dunia, huku wengine wanne wakinusurika kifo wakati wakishindana kunywa pombe kali baada ya kuahidiwa kupewa mkate, sukari na Sh50,000 kwa atakayeshinda. Moshi. Mtu mmoja amefariki dunia, huku wengine wanne wakinusurika kifo wakati wakishindana kunywa pombe kali, baada ya kuahidiwa kupewa mkate, sukari na Sh50,000 kwa atakayeshinda. Tukio hilo limetokea juzi katika kata ya Sanya Juu, wilayani Siha Mkoa wa Kilimanjaro, baada ya watu hao kuahidiwa na mtu anayedaiwa kuwa mfanyabiashara wilayani humo, ambaye sasa ametoroka. Inadaiwa kuwa mtu huyo aliwaahidi kuwapa zawadi hizo na mpaka mmoja anafariki walikuwa wameshakunywa chupa tano kati ya tisa zilizokuwa zikishindaniwa. Hata hivyo, baada ya kumaliza kunywa chupa tano hali zao zilianza kuwa mbaya na wengine kupoteza fahamu ambapo baadaye waliokolewa kwa kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Siha kupata msaada wa dharura. Mkuu wa wilaya ya Siha, Christopher Timbuka alimtaja aliyepoteza maisha kuwa ni Benson Mshi...

VIBANDA VYATEKETEA NA MOTO SOKO LA MLOWO CHANZO CHADAIWA JIKO LA KUKAANGIA SAMAKI

Picha
 Moto umeteketeza baadhi ya Vibanda katika soko la Magwaza lililopo Mlowo Wilayani Mbozi usiku wa jana  Jumamosi. Kwa mujibu wa mashuhuda wa moto huo wamedai chanzo cha moto huo kinaweza kuwa jiko la kuni ambalo hutumiwa na mama mmoja anaejihusha na ukaangaji wa Samaki. John Kabuje ambae anaishi jirani na soko hilo amedai kuwa usiku wa saa tatu kasoro usiku ndio moto huo ulipoanza kuibuka na ulianzia kwenye banda la mama mkaanga samaki na hatimae kushika vibanda vingine. "Bahati nzuri walikuwepo baadhi ya wateja wa vinywaji vya kilevi walikuwa wanakunywa ndani ya soko hili waliwahi kuona moto huo kabla haujaleta madhara makubwa"alisema shuhuda Kabuje Kwa upande wa Mwenyekiti wa soko hilo Tumaini Kabuje amesema chanzo cha moto huo ni jiko la samaki na jumla ya vibanda vilivyoathirika ni  vitatu pamoja cha kibanda chenyewe cha Mama muuza samaki Aidha Mwenyekiti huo amesema kuwa kumekuwepo na tabia  baadhi ya wakaanga samaki sokoni hapo kukaangia samaki wao ndani ya vib...

BUNGE LAPITISHA AZIMIO LA MKATABA DP WORLD

Picha
  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha azimio kuhusu pendekezo la kuridhiwa kwa mkataba baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kwa lengo la kuanzisha ushirikiano katika uendelezaji wa maeneo ya bandari nchini. Pendekezo hilo lililowasilishwa bungeni leo Jumamosi Juni 10, 2023 limepitishwa na Bunge baada ya wabunge kupata fursa ya kuchangia na kuishauri Serikali kuhusu mkataba huo. Kabla ya wabunge kuchangia, Waziri wa Ujenzi na uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alipata nafasi ya kuuelezea mkataba huo na manufaa yake kwa Taifa na kufafanua hoja zilizoibuliwa na wadau ikiwemo ya muda wa utekelezaji wake. Kamati ya Bunge ya Miundombinu, pia ilitoa ushauri wake kwa Serikali ikiwemo kuzingatia suala la ukomo wa muda katika mikataba itakayoingiwa, jambo ambalo linalalamikiwa na wadau kwamba makubaliano hayo hayajaonesha ukomo wa muda. “Waheshimiwa wabunge wanaoafiki hoja iliyowasilishwa kwetu na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi kuhusu pendekezo la kuridhiwa kwa mka...

BARABARA YA ILOLO-NDOLEZI YAWAIBUA WANANCHI MBOZI

Picha
 Mbozi. Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe wamesema ujenzi wa barabara ya Ilolo-Ndolezi utafungua fursa mbalimbali huku wakimshukuru Rais Samia Suluhu Hasan kwa kutoa fedha za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.  Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 11.01 inajengwa kwa gharama ya Sh6.46 bilioni fedha kutoka Serikali Kuu ambapo ikikamilisha itarahisisha usafiri, usafirishaji wa mazao, pembejeo za kilimo, utalii na kukuza uchumi wa eneo hilo. Wakizungumza na waandishi wa habari baadhi ya wananchi wanaoishi katika maeneo ambayo barabara hiyo inapita wamesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo utakuwa mkombozi kwa kuokoa gharama kubwa walizokuwa wanatumia awali hasa katika kusafiri. Mkazi wa Kitongoji cha Mzunguko Kata ya Mlowo, Mariamu Twinzi ameeleza kuwa barabara hiyo ikikamilika watasafiri kwa gharama nafuu. "Mimi naona barabara hii ikishakamilika tutasafiri kwa nauli nafuu. Tunamshukuru Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan kwa kutuona maana hii ilikuwa kam...

DC AWATAKA SKAUTI KUFANYA KAZI KWA WELEDI KWANI NDIO SIRI YA MAFANIKIO YAO

Picha
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi (DC), Esther Mahawe amewataka wahitimu wa mafunzo ya skauti wilayani humo kuweka vizuri njozi zao na kutamani kuwa watu wa viwango vya juu bila kujali hali za maisha walizotoka katika familia zao. Pia, amewaasa kuwa kufanya kazi kwa bidii na nidhamu ni nguzo ya mafanikio katika maisha. Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza hayo leo Alhamisi Juni 8, 2023 wakati akifunga mafunzo ya skauti  katika wilaya hiyo. Jumla ya vijana 119 walioweka kambi katika Shule ya Sekondari Vwawa  wamehitimu mafunzo ya skauti kutoka katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo. Akihitimisha mafunzo hayo, DC Mahawe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo amewaambia wahitimu hao "Hata ninyi mnaweza haijalishi background za familia zenu, iweke vizuri njozi kuwa unataka kuwa nani badaye,  Nakuhakikishi ukimuomba Mungu, ukifanya kazi kwa bidii, ukisoma kwa bidii utaishika njozi yako ndani ya muda mfupi sana" amesema  Amesema ili waweze kufanikiwa wanapaswa kutamani kuwa watu wa v...

STAMICO WAPONGEZWA KUSAIDIA HUDUMA ZA JAMII ILEJE

Picha
Mkuu wa wilaya Ileje mkoani Songwe Mhe. Farida Mgomi amelipongeza shirika la madini Tanzania STAMICO kupitia mgodi wa Kiwira_Kabulo Kwa kusaidia wananchi wanaouzunguka mgodi huo Kwa kuwapatia huduma jamii. Mhe. Mgomi ametoa pongezi hizo Juni 8,2023 wakati wa ziara ya siku Moja ya kutembelea migodi ya Kabulo na Kiwira yanakochimbwa makaa ya mawe ambapo alipokea taarifa ya maendeleo ya uzalishaji mkaa huo. Mhe.Mgomi amesema licha ya mgodi wa Kiwira _ Kabulo kukumbwa na changamoto ya mda mrefu ya kutozalisha makaa ya mawe wamejitahidi kushirikiana na jamii inayowazunguka Kwa kuwasaidia kusogeza huduma za  jamii. Mhe. Mgomi amesema uwepo wa migodi hiyo umewanufaisha wakazi wa Kijiji Cha Kapeta kata ya Ikinga wilayani humo, kwa kujengewa huduma za jamii ikiwepo kujengewa kituo Cha afya, kupelekewa huduma ya maji, kukarabati kituo Cha Polisi, nyumba za watumishi na miundombinu ya mgodi. "Niwapongeze Sana STAMICO Kwa uwekezaji wenu kwani mmeacha alama kubwa sana kusaidia hii jamii kwani ...

RAIS MUSEVENI AKUTWA NA CORONA

Picha
  Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema ameambukizwa Covid-19 baada ya moja ya vipimo vitatu vilivyofanyiwa uchunguzi kubainika kuwa na virusi. Bw Museveni, ambaye alitoa hotuba ya hali ya taifa mapema Jumatano, alisema alijihisi kuwa na homa kidogo, hali iliyomfanya kupimwa. Katibu wa kudumu katika wizara ya afya, Diana Atwine, alisema rais amepata dalili za mafua lakini yuko katika hali nzuri na ataendelea na majukumu yake. Alisema rais atafuata taratibu za kawaida za kuzuia maambukizi ya ya Covid wakati akitekeleza jukumu lake. Uganda ilikuwa na baadhi ya nchi za barani Afrika zlizochukua hatua kali kudhibiti kusambaa kwa virusi wakati wa kilele cha janga hilo, ikiwa ni pamoja na amri ya kutotoka nje kwa muda mrefu na kufungwa kwa shule na biashara. Nchi hiyo iliondoa vikwazo hivyo mwezi Februari 2022.

DC ILEJE AHITIMISHA MASHINDANO YA UMISSETA NGAZI YA MKOA SONGWE.

Picha
Mkuu wa Wilaya ya Ileje mkaoni Songwe Mhe. Farida Mgomi amewataka wanamichezo kuvilinda na kuheshimu vipaji vyao Ili kujitengenezea uchumi na kuondokana na utegemezi kupitia michezo. Akizungumza na wanachezo ambao ni wanafunzi wakati akifunga mashindano ya UMISSETA ngazi ya mkoa Juni 5,2023  katika viwanja vya shule ya sekondari Ileje ambako mashindano yamefanyika kimkoa wilayani Ileje Mhe. Mgomi amesema wanatarajia mkoa huo unarudi na kombe la kitaifa kwani timu iliyochaguliwa itauwakilisha vyema mkoa. Mhe. Mgomi amewataka wanafunzi hao kucheza kwa bidii na nidhamu ili kupata wachezaji Bora Kisha timu Bora ya Mkoa wa Songwe itakayopelekea (kunyakua) kushinda Makombe Yote huko Tabora ambapo mashindano haya yatafanyika kitaifa. "Niwakumbushe kwamba michezo inaweza kukuinua kiuchumi kwani kwa ulimwengu wa sasa imekuwa ni ajira, hivyo msibeze vipaji vyenu bali viheshimuni na kuviendeleza", amesema Mgomi. Katika hatua nyingine Mhe.Mgomi amekabidhi vikombe Kwa timu wilaya zilizofa...

DC MAHAWE AONYA WANAOHARIBU VYANZO VYA MAJI

Picha
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, Esther Mahawe amewaagiza wananchi wa wilaya hiyo kutunza mazingira ikiwemo vyanzo vya maji ili kuwaponguzia adha wanawake ya kutafuta maji umbeli mrefu. Mkuu huyo wa Wilaya ametoa maagizo hayo leo Jumatatu Juni 5, 2023 wakati akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kiwilaya yamefanyika Kijiji cha Nambala kata ya Mlowo wilayani humo. Amesema kuwa maji yanapokuwa changamoto wanawake na watoto ndio wanaathirika kwa kiasi kikubwa hasa kwa kutafuta nishati hiyo. "Msisahau kuwa maji yanapokuwa changamoto wanamama na watoto ndio wanapata shida kwenda kutafuta maji"  Amesema lengo la Rais Samia Suluhu Hassan ni kumtua ndoo mama kichwani kwa kuwasogezea huduma ya maji karibu ili muda wanaotumia kutafuta maji wautumie kwenye shughuli za uzalishaji. "Maelekezo niliyotoa yazingatiwe, tutunze vyanzo vya maji".  DC huyo amesema kuwa wilaya hiyo ina bahati ya kuwa na vyanzo vingi vya maji lakini changamoto moja ni k...

UTEUZI:RAIS ATEUA MADAS NA WAKURUGENZI

Picha
 

DC ILEJE AAGIZA KUUNDWA KLABU ZA KUSIMAMIA MAZINGIRA MASHULENI

Picha
Katika kuhakikisha jamii inakuwa na elimu endelevu ya uhifadhi wa mazingira wilayani Ileje mkoani Songwe, mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Farida Mgomi ameagiza kuundwa Kwa klabu za mazingira kwenye shule za msingi na sekondari Kwa lengo la kuhamasisha uhifadhi wa mazingira. Mhe.Mgomi ametoa agizo hilo Julai 5, 2023 katika Kijiji cha Chitete kata ya Chitete wilayani humo wakati Dunia ikiadhimisha siku ya mazingira kwa mwaka 2023 iliyobebwa na kauli mbiu; "Tokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki" . Mhe.Mgomi amesema watoto wakijengewa uwezo wakiwa angali wadogo wanaweza kuwa chachu katika uhifadhi wa mazingira, hivyo tutarejesha uoto wa asili uliokuwepo Toka enzi za mababu zetu. "Hakikisheni hizi klabu zinaundwa Kwa Kila shule kama zilivyo klabu za kupambana na madawa ya kulevya, klabu ya kupambana na rushwa, ili pia klabu ya kupambana na mazingira itakapojengewa uwezo wa kujuwa madhara ya uharibifu wa mazingira utakuwa msaada wa kukabiliana na kutokea Kwa majanga", amesema ...

SONGWE YAANZA VYEMA UMITASHUMTA

Picha
  Mkoa wa Songwe umeyaanza vyema mashindano ya UMITASHUMTA yanayoendelea kitaifa Mkoani Tabora.Kwa Mujibu wa Afisa Elimu Mkoa wa Songwe Michael Ligola ambaye ameambata na timu nzima ya michezo yote ya Mkoa wa Songwe amesema mpaka sasa Mkoa wa Songwe umeanza vyema katika michezo mbalimbali Ifuatayo ni Michezo Mkoa wa Songwe ilioshinda katika Michezo iliofanyika jana asubuhi Matokeo ya mechi za asubuhi ni  Netball Songwe 17 katavi 14 Handball Wasichana Songwe 19 Mbeya 9 Handball wavulana Songwe 15 Iringa 14 Volleyball wavulana Songwe set 3 Kagera 2

WANANCHI WAMKATAA DIWANI

Picha
 Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Muwimbi kata ya Lumuli, wilayani Iringa wameamua wampinga Diwani wao Muwimbi Mlusi kwa utendaji usioridhisha huku wakidai kuwa katika kipindi chake cha uongozi, kata hiyo imerudi nyuma kimaendeleo. Iringa. Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Muwimbi kata ya Lumuli, wilayani Iringa wameamua wampinga Diwani wao Muwimbi Mlusi kwa utendaji usioridhisha huku wakidai kuwa katika kipindi chake cha uongozi, kata hiyo imerudi nyuma kimaendeleo.  Hata hivyo Diwani huyo, ameiambia Mwananchi Digital kuwa madai yote yanayoelekezwa kwake siyo ya yakweli na kwamba ni kikundi kidogo cha watu wachache wanaotaka kumchafua na kumharibia rekodi yake ya utumishi uliotukuka. Aliongeza kwa kusema kuwa yupo nje ya kituo chake cha kazi na kwamba kama waandishi wa habari wanaotaka kujua undani wa taarifa hizo basi wamsubiri mpaka atakapoitishisha mkutano wa hadhara ambapo pamoja na mambo mengine, atazungumzia jambo hilo. “Najua ni kikundi kidogo tu cha watu ambacho kinawa...

KLABU YA JOGGING MKOA WA SONGWE YAPATA UONGOZI

Picha
 Klabu ya joggingi Mkoa wa Songwe imefanikiwa kupata Viongozi wa muda watakao iongoza kupata usajili ya jogging hiyo. Afisa habari wa Klabu hiyo Rahimu Mohamed amesema Klabu ya jogging imefanikiwa kupata Viongozi wa ngazi mbalimbali  "Lengo letu ni kuwa na klabu kubwa Nyanda za juu kusini hivyo tumeanza kujipanga kujiendesha wenyewe kwanza kabla ya kupata ufadhili na tumefanikiwa kupata Uongozi wa muda utakao tuvusha katika usajili na mambo mengine yajayo"amesema Rahimu Viongozi hao ni kama ifuatavyao Mwenyekiti  Elautery Mremi Makamu Mwenyekiti  Mnas Chande Katibu  Charles mwamlima Msaidizi katibu Sophia Mwampamba MHASIBU Sesilia Mwalim Benedict  Msaidizi Pius Mbeya WAALIMU FEADA HAONGA Na Hassan Kisambu HABARI/HAMASA  RAHIM NZUNDA na RAMADHANI MPONDA URATIBU ENG SULEIMAN BISHANGA WALEZI NMB, na POLISI MSIMAMIZI MKUU/MSHAURI OFISI YA KATIBU TAWALA MKOA WA SONGWE

DC ILEJE AFUNGA MAFUNZO YA SKAUTI AWACHA NA UJUMBE WA KUPINGA UKATILI

Picha
  SKAUTI wilayani Ileje  Mkoani Songwe wametakiwa kuwa chachu ya uzalendo na kujituma kwenye jamii Kwa kukemea matukio ya ukatili kwa kuripoti kwenye mamlaka husika ikiwepo viongozi wa vijijiji, jeshi la polisi na ustawi wa jamii. Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Farida Mgomi amesema hayo Juni ,3,2023 wakati akifunga mafunzo ya skauti Kwa vijana 267 yaliyofanyika Kwa siku 5 katika shule ya sekondari Ndola iliyopo kata ya Ndola wilayani humo. Mhe. Mgomi amewataka skauti hao kuwa mabalozi wa kupinga ukatili Kwa kutumia mafunzo hayo waliyofundishwa kanuni, na taratibu za skauti Kwa lengo la kulisaidia taifa kukabiliana na matukio yasiyo mema Kwenye jamii. "Ukijifunza mafunzo ya Skauti huwezi kuwa lege lege na ni lazima utakuwa mzalendo na huwezi kukanyagwa na kuwa mkia bali utakanyaga na kuwa kichwa", amesema Mhe.Mgomi. Mhe. Mgomi amesema tuendelee kuishi na falsafa za mwanzilishi chama cha Skauti Ulimwenguni Sir.Rord Robert Stephenson Smyth "Baden Powell" februari 22 mwaka 18...