Machapisho

KAMANDA WA POLISI SONGWE APELEKA SOMO LA UKATILI WA KIJINSIA KANISANI TUNDUMA ATOA WITO

Picha
 Kamanda wa polisi mkoa wa songwe kamishna msaidizi wa jeshi la polisi Theopista Mallya ametembelea kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo chini ya mchungaji Edwine Sostenes katika mtaa wa Nyerere mjini Tunduma wilaya ya Momba mkoani Songwe Kamanda wa polisi mkoa wa songwe alipata nafasi ya kutoa elimu kwa waumini wa kanisa hilo Katika mambo mbalimbali ambayo yanapelekea matendo maovyo na kupelekea ukatili wa kijinsia na uhalifu, Ikiwa pamoja na Rushwa,Ulawiti,Tamaa ya mali,Kubaka,Wivu wa Mapenzi,Ushoga Migogoro ya ardhi, Ulevi uliokithili,Imani za kishirikina, Huduma za polisi ni bure,Kudhini na ndugu wa damu na pia Wananchi kushirikiana na jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu ili kutokomeza vitendo hivyo katika maeneo yao yanayowazunguka. Aidha elimu hiyo imetolewa kwa kutumia vifungu mbalimbali vya maandiko katika Biblia vinavyozungumzia mambo hayo, Sambamba na hayo aliyataja madhara ya vitendo hivyo ikiwa pamoja na Matatizo ya akili, ulemavu, kujitenga na marafi...

PAPII KOCHA AONDOKA TUKUYU SOUND NA KUJIUNGA TOWN CLASSIC

Picha
 Msanii wa Muziki wa Dansi Papii Kocha almaarufu kama mtoto ametua rasmi katika bendi ya Town Classic. Kwa mujibu wake Papii amesema kuwa ameamua kuondoka Tukuyu si kwa ubaya na tayari amewajulisha walezi wa bendi hiyo Alnanuswe Kabungo na Benjamini Mwandete pia amewaaga wanamuzi wenzie ikiwemo Mkurugenzi mwenzie Kalala Junior "Mimi nimeondoka kwa wema ndio maana niwaaga wote kwa wema  kuanzia walezi wangu mpaka wanamuzi wenzangu"-Papii Aidha Papii amewataka mashabiki wa Tukuyu kutomuona yeye ni adui kisa tu yeye kusaini mkataba na Town Classic ni kwamba ameamua kwenda kujifunza changamoto mpya za kimaisha. Nae mmoja wa walezi wa bendi ya Tukuyu sound Benjamin Mwandete amethibitisha kuondoka kwa Papii Kocha na wenzie watatu na amesema ni kweli wameondoka kwa kuaga na wamewapa baraka zote "Mwandishi haya ni maisha na wao wanatafuta maisha kama huko walikokwenda wameona kuna maslahi hakuna wa kupinga Papii ni mtoto wetu kaaga vizuri nyumbani na tumemwambia akiona hakuelewe...

RAIS SAMIA ATENGUA UTEUZI WA KATIBU WA WIZARA YA MAJI

Picha
 Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu Wizara ya Maji Nadhifa Kemikimba. Kemikimba aliteuliwa kushika nafasi hiyo  Februari 26, 2023 na aliapishwa kushika wadhifa huo katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma Februari 27, 2023. Awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo na amewahi pia kutumikia nafasi mbalimbali ikiwamo Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Ubora wa Maji. Taarifa ya kutenguliwa kwake imetolewa leo Ijumaa Agosti 18, 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zuhura Yunus

TANROADS SONGWE YAKAMILISHA UJENZI WA BARABARA MITA 500 CHITETE-MOMBA

Picha
  Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Songwe imekamilisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kipande cha mita 500 katika Mji wa Chitete Makao Makuu ya Wilaya ya Momba ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali kila Makao Makuu ya wilaya lazima miundiombinu iboreshwe. Msimamizi wa kitengo cha matengenezo ya barabara mkoa wa Songwe Mhandisi Silvan Henry Mloka amebainisha hayo Agosti 3, 2023 alipozungumza na kipindi cha TANROADS mkoa kwa Mkoa kwa niaba ya Kaimu Meneja wa TANROADS mkoa wa Songwe Mhandisi Suleiman Bishanga. Amesema katika mwaka wa fedha 2022/2023 kiasi cha fedha shilingi milioni 500 kilitengwa na Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, kuweka taa za barabarani, pamoja kujenga Makalavati kwa ajili ya njia za Maingilio. Mhandisi Mloka amesema mradi huo umetekelezwa na Mkandarasi mzawa wa kampuni ya GNMS CONTRACTORS CO LIMITED ya Iringa, am...

MAMA WA KAMBO AWANYWESHA SUMU WATOTO WA MUMEWE

Picha
 Watoto wawili wa familia moja, Dickson Zakaria (5) na Goodluck Zakaria (4) wamefariki baada ya mama yao wa kambo kuwanywesha dawa ya kuulia wadudu kwenye mazao. Akizungumza Agosti 14, 2023, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amesema tukio hilo limetokea Agosti 12, 2023 saa tatu usiku katika kijiji na kata ya Itobo Wilaya ya Nzega. Amesema watoto hao walikorogewa sumu na mama huyo (jina limehifadhiwa) kisha nayeye kunywa sumu hiyo. Abwao ametaja chanzo cha tukio hilo ni baada ya baba wa watoto hao aitwaye Zakaria Dotto kudaiwa kutotoa fedha za matumizi na kusababisha mzozo uliopelekea kukimbia kuukwepa. Kitendo hicho kinadaiwa kumuudhi mama huyo aliyeamua kukoroga sumu ya dawa ya kuulia wadudu kwenye mazao na kuwanywesha watoto hao na yeye kuinywa. Baba wa watoto hao aliporudi nyumbani kwake alikuta hali ya mkewe si nzuri ndipo alipomkimbiza hospitali pasipokujua chochote kuhusu watoto wake. "Alimkuta mkewe katika hali isiyo nzuri baada ya kunywa sumu na kumpeleka hos...

WANNE MBARONI KWA MAUAJI

Picha
 Watu watatu wametuhumiwa kumnyonga mtu na kumkata shingoni yake na kitu chenye ncha kali na wengine watano akiwemo mwanamke wanatuhumiwa kwa kumpiga hadi kufa mtu aliyedaiwa kuiba mahindi akiwa shambani. Kiteto. Watu watano wamesomewa shitaka la mauaji ya Amos Ephael (69) mkazi wa Kijiji cha Kazingumu, Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara kwa tuhuma za mauaji. Akisoma shitaka hilo Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Boniphace Lihamwike leo Agosti 14, 2023 amesema watuhumiwa hao kwa pamoja wametenda kosa hilo kinyume na kifo cha 196 kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2022. Hakimu Lihamwike amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Jastini Emmanuel (42) mkazi wa Kazingumu na mtu mwingine aliyejulikana kwa jina la Pima Peter (27) mkazi wa Langtomon, Wengine ni Hamis Husein (24) mkazi wa Kibaya, Peter John (47) mkazi wa Langtimon na Neema Emmanue (27) mkazi wa Kazingumu. Imeelezwa mahakamani hapo kuwa watuhumiwa hao kwa pamoja walimpiga na kumsababishia kifo Amos Ephael (69) ...

DC ILEJE AWATAKA WAMAMA KUTENGA MUDA KUWANYONYESHA WATOTO

Picha
MKUU wa wilaya ya Ileje mkoani Songwe Mhe.Farida Mgomi ametoa rai kwa jamii wakiwemo waajiri na kinababa Mkoani humo kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kinamama wanaonyonyesha watoto ili waweze kuwanyonyesha watoto wao katika hali ya utulivu ikiwemo  kuweka mazingira wezeshi ili unyonyeshaji huo ufanyike kwa  tija kwa watoto. Mhe. Mgomi ametoa rai hiyo Agosti 7,2023 wakati akiwasilisha hotuba katika kilele Cha wiki ya unyonyeshaji kimkoa akimwakilisha mgeni rasmi ambaye alikuwa mkuu wa mkoa wa Songwe Dkt. Francis Michael ambayo kimkoa imefanyika katika kijiji Cha Msia kata ya Chitete wilayani Ileje. Mhe. Mgomi amesema ili unyonyeshaji ukamilike lazima kuwe na usaidizi upande mwingine ,ambapo pia mama anajukumu la kunyinyesha Kila siku nakupanga majukumu yake vizuri. "Kuna kila sababu wababa(waume) kusaidia unyonyeshaji kwani suala la unyonyeshaji sio la baba na mama bali jamii kwa ujumla kwani mtoto anatakiwa kupata maziwa ya mama tangu anapozaliwa mpaka miaka 2," amesema Mhe.M...

KIGAHE: TRA WAFUATENI WAFANYABIASHARA MAENEO YAO MUWAPE ELIMU

Picha
   Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amewataka watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Songwe kuwafwata wafanyabiashara kagika maeneo yao ili kuwapa elimu na kujadiliana namna ya kulipa kodi badala ya kuwasubiria wafanyabiashara kuja ofisini. Kigahe ameyoa agizo hilo leo Jumatano Agosti 10, 2023 wakati wa mkutano wake na  baadhi ya  wafanyabiashara wa mkoa huo mjini Vwawa. "Mimi nadhani muende katika maeneo yao ya biashara badala ya kuwasubiri wafanyabiashara kuja ofisini" amesema na kuongeza; "Tutoke tukawaelimishe watu. Naona mkienda katika maeneo ya wafanyabiashara mtatoa elimu na kukubaliana namna ya kupanga kodi na utaratibu huo utakuwa na matokeo chanya" amesema  Akizungumza katika mkutano huo Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Songwe, Aderick Alphonce  amesema kuwa wamepokea maagizo hayo na wanakwenda kuyafanyia kazi. "Kuanzia sasa tutakuwa tunakuja katika biashara zenu kutoa elimu na msiwaogope maofisa wa TRA" ameahidi Kaimu ...

TASISISi ZA SERIKALI ZATAKIWA KUBORESHA HUDUMA KUVUTIA SEKTA BINAFSI

Picha
Songwe. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amezitaka taasisi za Serikali kuboresha huduma ili kuwezesha sekta binafsi kufanya biashara mipakani kwa uhuru. Naibu waziri huyo ameyasema hayo leo Jumatano Agosti 9, 2023 wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani Songwe. "Nipo hapa kwaajili ya mpango wa kuboresha mazingira ya sekta binafsi ambayo ni maelekezo ya Rais Samia kuboresha sekta binafsi ambayo ni injini ya uchumi wa Tanzania na Dunia kwa ujumla" amesema  na kuongeza; "Ujue wa sekta binafsi ikisimamiwa vizuri inafanya vizuri.Tunataka kuona taasisi za Serikali zinawezesha taasisi binafsi kupata huduma bila vikwazo ili kurahisisha ufanyikaji wa biashara katika mpaka wa Tunduma"  Kigahe amewaagiza wakala wa vipimo kukagua bidhaa ili kupata thamani ya kilichofungashwa. "Mkuu wa mkoa wa Songwe ametupa ushirikiano ambapo tunaona wakulima watapata stahiki zao kwa kupima uzito ulio sahihi kwa mizani tofauti na sasa wanavyotumia BP, ndoo na lumbesa...

JKT WAKABIDHIWA VIJANA WA BBT KUWAFUNDA UKAKAMAVU NA UZALENDO

Picha
  WAZIRI wa Kilimo, Hussein Bashe amesema z vijana 812 wanaotarajiwa kuhitimu mafunzo ya BBT mwaka huu wanatarajiwa kunolewa kuhusu masuala ya uzalendo na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Mkataba wa makubaliano kuhusu mafunzo hayo ya mwezi mmoja yamesainiwa leo na kushuhudiwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kilele cha maonesho ya wakulima Nane nane yaliyofanyika kitaifa kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya. Vijana hao waliokuwa katika vituo atamizi 13 kwa kipindi cha miezi mine, tarehe 20 Agosti mwaka huu wanatarajiwa kukodishiwa mashamba kwa miaka 66 ili kuendeleza shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji baada ya kupatiwa mafunzo hayo. Amefafanua kuwa Serikali inaendelea kuwatafutia wawekezaji watakaonunua mazao yatakayozalishwa kwenye mashamba hayo ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba katika mashamba hayo. Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli amesaini hati ya makubalino na Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa ajili ya ushirikiano katika kuwaendeleza vijan...

BASI LA GOLDEN DEER LAPINDUKA

Picha
 Mtu mmoja amelazwa katika Hospitali ya Mtakatifu Kizito wilayani Mikumi na wengine wametibiwa na kuruhusiwa baada ya basi la kampuni ya Golden Deer walilokuwa wakisafiria kutoka Kyela kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka. Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Alex Mkama amesema kuwa ajali hiyo imetokea leo Jumatatu Agosti 7, 2023 jioni eneo la Msimba kwenye mteremko na kona za Iyovi Mikumi ambapo amemtaja majeruhi kuwa ni Elinipenda Kishimbo (26) aliyeteguka mkono. Kamanda Mkama amemtaja dereva wa basi hilo kuwa ni George Obedi (48) huku chanzo cha ajali hiyo kikitajwa kuwa ni uzembe wa dereva huyo kwa kuwa alitaka kulipita gari lililokuwa mbele yake bila ya kuchukua tahadhari na hivyo kukutaka na gari jingine uso kwa uso "Huyu dereva bila kujali kuwa eneo lile ni hatari alilipita gari lililopo mbele na kabla hajalipita likatokea gari jingine mbele alichoamua ni kwenda kulia zaidi mwa barabara na hivyo alishindwa kulimudu basi hilo hasa ukizing...

MTANZANIA ATEKWA NIGERIA,WATEKAJI WATAKA MAMILIONI

Picha
 Mtanzania ambaye ni frateri wa Shirika la Wamisionari wa Afrika (White Fathers) mzaliwa wa Parokia ya Kabanga, Jimbo la Kigoma, Melkiori Mahinini (27) ametekwa nyara na watu wasiojulikana nchini Nigeria. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Kigomba, Joseph Mlola, mseminari huyo alikamatwa Agosti 4 mwaka huu katika jimbo la Minna huko Nigeria akiwa na mwenzake, Padri Paul Sanogo, raia wa Burkina Faso. “Walitekwa na kundi la watu wasiojulikana mapema usiku wa kuamkia Agosti 3, 2023 katika Parokia ya Mtakatifu Luka Gyedna, jimbo la Minna nchini Nigeria. Mseminari wetu huyu alikuwa katika mwaka wake wa uchungaji kabla ya kuanza masomo ya teolojia “Tumwombe Mungu asikilize sala zetu na awanusuru katika hatari zozote na awarudishe katika amani, mwanga na uhuru kamili,” alisema Askofu Mlola katika taarifa yake kwa waumini na Taifa kwa ujumla. Kufuatia ya taarifa hiyo ambayo imesambaa pia mitandaoni, gazeti hili lilimtafuta Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Dk...

DC ILEJE AWATAKA WANANCHI KUTUNZA MIUNDOMBINU NA KUOMBA UMEME

Picha
Mkuu wa wilaya ya Ileje mkoani Songwe  Mhe. Farida Mgomi amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kutunza na kulinda miundombinu ya umeme huku akiwataka kuhakikisha wanatumia umeme kwa usalama. Mhe. Mgomi ametoa rai hiyo Agosti 4, 2023  wakati mwenyekiti wa bodi ya wakala wa nishati vijijini REA Janeth Mbene katika vijiji vya Ibandi kata ya Kalembo na Kijiji cha Shinji Kata ya Mbebe akizindua mradi wa nishati mzunguko wa pili katika kata hizo. Mhe. Mgomi amesema kama umeme umefika kwenye vijiji vyao mnatakiwa kubaini fursa zinazoweza kuwaingizia kipato kwenye maisha ya kila siku. "Tumeona serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan  imetoa fedha nyingi sana itashangazwa tuanfurahia tu kuwaka kwa taa ,badala ya kujitengenezea miradi itakayotumia nishati hiyo", amesema.Mhe. Mgomi. Mhe.Mgomi amezitaka halmashauri za vijiji kuhakikisha tunatunza miundombinu ya umeme ikiwepo kudhibiti kuchoma moto na kuharibu nguzo ni marufuku. "Ni marufuku kuona nguzo zina...

DC MAHAWE AWAITA WANAMBOZI KUJIFUNZA NANENANE MBEYA

Picha
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Esther Mahawe ametoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo na Mkoa wa Songwe kwa ujumla kushiriki katika maonyesho ya kilimo, ufugaji na uvuvi maarufu Nanenane ili waweze kujifunza mambo mbalimbali. Amesema kuwa maonyesho hayo yana lengo la kuwapa elimu wananchi katika sekta ya kilimo, ufugaji na uvuvi hivyo watumie fursa hiyo kutokana na wilaya hiyo kujihusisha na kilimo kwa asilimia kubwa na hakuna kiingilio. "Niwasihi wananchi wa Mbozi na Mkoa wa Songwe kwa ujumla wafike kwenye maonyesho haya ili waweze kujifunza. Kuna mambo mengi ambayo wakifika watonufaika, maonyesho ya mwaka huu yamekuwa tofauti hivyo wakija hawataondoka bure" amesema    Akiwa kwenye banda la maonyesho la Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi leo Ijumaa Agosti 4, 2023 Mkuu huyo wa Wilaya ya Mbozi ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dk Francis Michael katika maadhimisho hayo amebainisha kuwa wananchi watapata firsa ya kuona mbegu bora za mazao na mifugo, kujifunza mbinu za kilimo na...

TAKUKURU SONGWE YATOA TAARIFA YAKE YA MIEZI MITATU

Picha
Taasisi ya Kuzuai na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Songwe imewataka wananchi katika mkoa huo kutoa ushirikiano wa taarifa za rushwa kwa kuwa ipo sheria ya kuwalinda watoa taarifa hizo. Pia, imesema kuwa zipo sheria ambazo zinawabana maofisa wa taasisi hiyo kutoweka wazi wanaowapa taarifa za rushwa hivyo wananchi wasiogope kutoa taarifa pale wanapobaini kuwa kuna viashiria vya rushwa hasa kwenye miradi ya maendeleo. Hayo yamesemwa leo Alhamisi Agosti 3, 2023 na Mkuu Takukuru Mkoa wa Songwe, Edings Mwakambonja wakati akitoa taarifa ya ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni mwaka huu kwa waandishi wa habari. Amesema kuwa Takukuru Rafiki imesaidia kuiweka taasisi hiyo karibu na wananchi kutokana na elimu wanayoitoa ambayo imesaidia wananchi kuondoa hofu. “Katika kipindi cha Aprili mpaka Juni tumefanikiwa kufika katika kata 15 kutoa elimu na kusikiliza kero za wananchi. Kero 84 zilitolewa na kati ya hizo kero 41 zilishatatuliwa na zilizobaki zinaendelea kush...

ALIEKUWA DC MBARALI MAHAKAMA YAMUACHIA HURU

Picha
 Mahakama ya wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi imemuachia huru aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Reuben Mfune na mwenzake waliokuwa wanakabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi Uamuzi huo umetolewa Leo August 3, 2023 na hakimu Mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya hiyo Mariamu Mchomba baada ya Mkurugenzi wa mashtaka nchini (DPP) kuielezea mahakama kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo Inadaiwa kuwa Reuben Mfune na mwenzake walikuwa wanakabiliwa na kosa la uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya shilingi Milioni 51 ambapo Katika kipindi hicho Mfune alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ruangwa kuanzia 2012 - 2015 Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) ameifuta kesi hiyo Kwa *NOLLE PROSEQUI* chini ya kifungu 91(1) Cha sheria ya mwenendo wa Makosa ya jinai sura ya 20 kama ilivyorekebishwa mwaka 2022 ambayo iliwasilishwa na wakili wa Serikali mwandamizi Mwanaamina Kombakono

ZIARA YA AWESO SONGWE AAGIZA KUUNDWA MAMLAKA YA MAJI

Picha
 WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amemuagiza Mkurugenzi wa Idara ya Usambazi Maji Vijijini ,Joyce Msiru kwa kushirikiana na watendaji wengine katika Wizara hiyo kuanza mara moja mchakato wa kuunda mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Mkwajuni ili kurahisisha utendaji na kufikisha huduma ya maji kwa wananchi. Ametoa agizo hilo, Julai 31,mwaka huu katika siku yake ya kwanza ya ziara ya siku mbili mkoani hapa mara baada ya kupokea taarifa ya hali ya upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Songwe. Katika taarifa hiyo ya upatikanaji wa maji ilieleza kuwa Kata za Mkwajuni na Saza ambazo zina idadi ya wakazi wasiopungua 40,000 hivyo kunahitajika msukumo wa ziada wa upatikanaji wa maji.         Kutokana na hali hiyo, Waziri Aweso amesema kwa kuanzia Wizara itapeleka kiasi cha milioni 500 ili kuanzisha mamlaka hiyo ikiwemo na shughuli zingine. ” Mkurugenzi wa idara ya usambazi maji vijijini ‘Msiru” pamoja na viongozi wa Ruwasa Mkoa mnatakiwa kubaki hapa ili kuanza mc...

MKURUGENZI TUNDUMA ATANGAZA MIKAKATI ZAIDI KUINUA MAPATO YA NDANI.

Picha
HALMASHAURI ya Mji Tunduma, Wilaya ya Momba, Mkoani Songwe ipo kwenye mchakato wa kufanya upanuzi wa Maegesho (Truck’s Parking) ya magari makubwa yanayovuka mpaka wa Tanzania na Zambia, kutoka magari 120 hadi malori 300 kwa lengo la kusisimua na  kuiongezea Halmashauri hiyo mapato yake ya ndani. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Philemon Magesa, katika mahojiano maalum na gazeti hili yaliyolenga kupata taarifa zinazohusiana na utekelezaji wa mikakati ya ukusanyaji wa mapato ya ndani na kusababisha mapato hayo kuongezeka mara dufu. Moja ya Malori ya Mizigo likiingia kupaki katika maegesho ya Halmashauri ya Tunduma.  Halmashauri ya Mji Tunduma imeongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali, ikiwemo miradi ya kimkakati na kufikia kiasi cha shilingi bilioni 13.7 kwa mwaka. Akifafanua zaidi kuhusu utekelezaji wa mradi huo wa upanuzi wa maegesho ya magari makubwa yanayovuka Mpaka wa Tanzania na Zambia (Truck’s Parki...

NGASA AFUNGWA MAISHA KWA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA 4 HADHARANI

Picha
 Mkazi wa Kijiji cha Madoletisa Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora, Ngasa Polepole (19) amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani baada ya kutiwa hatiani na Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Sikonge kwa kosa la kumlawiti mtoto wa kiume mwenye miaka minne. Hukumu hiyo imetolewa Julai 27, 2023 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Irene Lyatuu baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo. Katika shauri hilo namba 13/2023 upande wa Jamhuri ulikuwa na mashahidi sita huku mshitakiwa akisimama mwenyewe kwenye utetezi kujitetea. Hakimu Lyatuu amesema Mahakama imejiridhisha pasipokuwa na shaka yoyote kwamba mshitakiwa Ngasa Polepole amehusika moja kwa moja kutenda kosa hilo la udhalilishaji kwa mtoto wa miaka minne ambaye jina limehifadhiwa. “Baada ya kupitia mwenendo wa shauri hili na ushahidi uliotolewa, Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa na kumhukumu kifungo cha maisha,”amesema Awali Wakili upande wa Jamhuri, Joseph  Mwambwalulu  aliiambia Mahakama kuwa Ngasa a...

DC MBOZI AKABIDHI PIPA TAKA VWAWA NA MLOWO TOKA TANROADS

Picha
  Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Ester Mahawe amekabidhi mapipa taka katika miji ya Mlowo na Vwawa yaliotolewa na Wakala wa barabara Tanzania ( Tanroads) kupitia Vikundi vya vinavyofanya wa barabara kuu ya Tanzam. Ugawaji huo umefanyika siku ya jana kwa kuanza na mji wa Mlowo stendi ya Zamani ambapo Mkuu wa Wilaya akiwa ameongozana na kamati ya usalama ya Wilaya na Viongozi toka Tanroads wakiongozwa na kaimu Meneja Injinia Suleiman Bishanga walikabidhi vifaa hivyo ambavyo vitawekwa kenye maeneo mbalimbali mji wa Mlowo Diwani wa kata ya Mlowo  Jaksoni Mwanda amewashukuru Tanroads kupitia vikundi kwa kuwapatia mapipa hayo kwani wao kama mamlaka ya mji wapo katika mipango ya kuuweka mji huo safi na Vifaa hivyo kwao wanaona ni kama neema iliokuja wakati mwafaka.  ( Mkuu wa Wilaya Mbozi akiwa katika picha ya pamojo na vikundi vya usafi) Wakiwa katika stendi ya mji wa Vwawa ambapo ugawaji huo umefanyika zilipo ofisi ya kata ya Ichenjezya Bahati Mbugi Diwani wa Ichenjezya akiongea kwa ...

POLISI SONGWE YAWASAKA WALIOFANYA MAUAJI MBOZI

Picha
 Watu wawili wamekutwa wameuawa katika matukio mawili tofauti katika vijiji vya Bara na Igamba wilayani Mbozi, Mkoa wa Songwe. Wakati mmoja akikutwa amekutwa amechinjwa, mwingine amekatwa kichani na kitu kinachosadikiwa kuwa na ncha kali. Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani, hapa Rashid Ngonyani amesema leo Jumanne Julai 25 mwaka huu kuwa Jeshi la polisi mkoani hapa, linawasaka watuhumiwa wa makosa mawili tofauti ya mauaji, ambayo yametokea hapa mkoani Songwe. Ameelezea tukio la kwanza kuwa lilitokea Julai 22, 2023 saa 21:00 usiku katika kijiji cha Twinzi wilayani hapa, Mwanamke mmoja Hilda Mwambughi (73), mkazi wa kijiji hicho alikutwa ameuawa nyumbani kwake kwa kukatwa kichwani na kitu chenye ncha kali, na watu wasiofahamika ambao waliomvamia nyumbani kwake na kutekeleza tukio hilo. "Chanzo cha tukio hio hakijafahamika na uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea, na kwamba jeshi la polisi mkoani Songwe linaendelea kuwasaka watuhumiwa wa tukio hilo la mauaji," amesema Ngonyani. Ng...

MLINZI WA DC ADAIWA KUUWAWA NA DEREVA BAJAJ

Picha
 Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 55, alikuwa ni askari wa Jeshi la akiba (Mgambo), na alifariki dunia Julai 21, mwaka huu baada ya kujeruhiwa na Abdi (21) na hivyo kusababisha kifo chake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema lilitokea Julai 21, saa 6:30 mchana maeneo ya Majengo kwa Mchomba, baada ya mtuhumiwa huyo kukataa kukamatwa kwa kosa la kufanya fujo na kuwatishia ndugu zake. Samia aweka jiwe la msingi mnara wa mashujaa Kitaifa 20 min ago "Tukio hili limetokea Julai 21, 2023 majira ya saa 6:30 mchana huko maeneo ya Majengo kwa Mchomba, Kata ya Majengo, Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, ambapo marehemu alijeruhiwa na kitu chenye ncha kali ubavuni na mtuhumiwa huyo," amesema na kuongeza; "Kufuatia tukio hili, tunamshikilia Abdan Mohamed Abdi, (24), dereva bajaji kwa tuhuma za kusababisha kifo cha Michael Dastani Ngulizi, (55), askari wa Jeshi la Akiba (Mgambo) ambaye pia ni mlinzi wa ofisi ya Mku...

DIRA YA MAENDELEO TAIFA 2050 YAJADILIWA SONGWE

Picha
 Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dk Fransis Michael ameongoza Semina ya Mafunzo elekezi ya maandalizi ya dira ya taifa ya maendeleo 2050  kwa watumishi wa Umma katika ukumbi wa Mkoa uliopo katika jengo la ofisi yake Wilayani Mbozi.  Akiongea katika ufunguzi Mkuu wa Mkoa amewataka wajumbe wa Semina hiyo iliowashirikisha wakuu wa Wilaya, Madas,Wakurugenzi wa halmashauri, Wakuu wa wa taasisi za fedha,Mameneja taasisi za Umma Viongozi wa Dini, Viongozi wa vyama vya Siasa na Wataalamu mbalimbali toka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe  kusikiliza  na kutoa maoni yao kwani ndio dira ya maendeleo ya  Taifa hivyo kutoa kwao maoni ndio mafanikio ya Nchi.  ( Meneja Tanroads na Meneja Tanesco wakifuatilia kwa makini semina hiyo) "Niwaombe Viongozi wenzangu leo tumepata ugeni toka Wizarani kwa lengo la kutoa semina ya dira ya maendeleo kwa ustawi wa Nchi yetu hivyo tuwasikilize na kutoa maoni yetu kwani ni muhimu sana katika kulipeleka taifa letu mbele"amesema Dkt Michael Sem...