MWALIMU ADAIWA KUMLAWITI MWANAFUNZI CHOONI
Baada ya kusambaa video mtandaoni, akimuonesha mtoto darasa la tatu akisimulia namna alivyofanyiwa ukatili na mwalimu wake, Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima amesema hatua zimeshachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa. Dk Gwajima ametoa majibu kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter,akiandika "shtaka la mtuhumiwa lipo polisi RB namba ARS/RB/3429/2023. Wako watoa huduma ambao wamevaa vazi la kondoo kumbe ni wanyama wakali dhidi ya watoto . Wazazi semeni na watoto msisubiri tukio limkute, semanae sasahivi hapo ulipo 'mwanangu marufuku mtu kuleta agenda za kugusa mwili wako wala kupita pembeni na kukueleza lolote kukuambia usiseme wala asikutishe ukanyamaza piga kelele toa taarifa'"aliandika. Hata hivyo katika maelezo yake amependekeza mbinu mpya kwa jamii, watoto kuwa na filimbi wakiona dalili za hatari ya mtu kutaka kushika mwili wake wapulize, kama mkakati moja wapo wa kukabiliana na vitendo hivyo. Kwa uchache katika vid...